Mwamba house tunawasaidia watoto yatima ambao wameachwa na wazazi wao kwa ajili ya mlipuko wa ugonjwa wa ukimwi na pia watoto wa mitaani na watoto wanaoishi katika mazingira magumu au hatarishi na watoto ambao hawapati au wanapata ziada kidogo katika elimu na afya.
Kwa sasa tunawafundisha watoto katika eneo la nyasaka Mwanza. Tuna watoto wa kuanzia umri wa miaka mitano (5) hadi kumi na tatu (13). Miongoni mwa wototo hawa wengi wao hawajawahi kuhudhulia shule kabisa kwa sababu ya kukosa fedha za kununua vifaa vya elimu kama vile sare ya shule n.k.

Kwa sasa tuna wafundisha watoto hawa katika nyumba ambayo haijaisha kwa huruma tumeruhusiwa na mwenye nyumba kama darasa tukiwa tunasubili ujenzi wa kituo.